Neymar amezidi kutikisa vichwa vya
habari baada ya kufunga magoli mawili na kusaidia kutoa nafasi za
kufunga wakati Paris Saint-Germain ikiichakaza Toulouse magoli 6-2.
Katika mchezo huo Max Gradel alikuwa
wa kwanza kuipatia Toulouse goli la kushtukiza dhidi ya Paris
Saint-Germain katika dakika ya 18 jana usiku.
Lakini Neymar alisawazisha goli hilo
dakika 13 baadaye kisha Adrien Rabiot kuongeza goli la pili
akisaidiwa na Neymar huku Edinson Cavani akiongeza goli la tatu kwa
mkwaju wa penati.
Toulouse ikapata goli la pili
kupitia kwa Thiago Silva aliyejifunga, hata hivyo PSG wakaongeza
magoli mengine kupitia kwa Javier Pastore, Layvin Kurzawa na Neymar.
Mshambuliaji nyota wa PSG Mbrazili Neymar akiachia shuti na kufunga goli
Mbrazili Neymar akitumbukiza goli lake la pili katika mchezo huo walioibuka na ushindi mnono
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni