Mchezaji anayeondoka Chelsea Diego
Costa amekwea pipa akitokea Brazil kwenda Hispania akitarajia
kujiunga tena na klabu yake ya Atletico Madrid kwa dau nono.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa
Hispania amesema hana kinyongo na kocha Antonio Conte, licha ya kocha
huyo kumtumia arafa isemayo hana mpango naye.
Hatimaye Costa amekubali kurejea
kwenye klabu yake hiyo ya zamani ya Atletico, ambapo uhamisho wake
utakamilishwa Januari, baada ya kuondolewa katazo la kusajili La
Liga.
Diego Costa akiagana na watu katika uwanja wa ndege wa Brazil kabla ya kupanda ndege kuelekea Hispania
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni