Riyad Mahrez ameiokoa Leicester City
kuambulia pointi nyumbani baada ya kufunga goli la kusawazisha katika
dakika ya 80 na kufanya matokeo kuwa 1-1 dhdi ya West Bromwich
Albion.
Wageni West Bromwich Albion walikuwa
wa kwanza kufunga goli kupitia mpira wa adhabu uliopigwa na Nacer
Chadli na kuonekana kwamba huenda goli hilo lingewapa ushindi.
Lakini Mahrez aliyepoteza nafasi
nyingi za kufunga wakati ambapo matokeo yakiwa 0-0 aliifungia
Leicester City goli la kusawazisha likiwa ni goli lake la kwanza
katika msimu huu.
Mpira wa adhabu uliopigwa na Nacer
Chadli ukielekea kujaa wavuni
Riyad Mahrez akifunga goli la kusawazisha la Leicester City
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni