Kocha wa Manchester United, Jose
Mourinho amesema kikosi chake kilipaswa kufunga magoli 6 katika
kipindi cha kwanza katika mchezo waliofungwa goli 1-0 na Basel.
United walikitawala kipindi cha
kwanza katika mchezo huo waliokuwa ugenini huku Marouane Fellaini
pamoja na Marcos Rojo mashuti yao yakigonga mwamba.
Mchezaji wa Basel Michael Lang akifunga goli pekee katika mchezo huo
Lionel Messi alianzia benchi wakati
Barcelona wakitinga hatua ya 16 bora baada ya kutoa sare tasa kwa mara ya pili katika hatua ya makundi.
Sare ya mchezo wa Oktoba dhidi ya
Olympiakos ilikuwa ya kwanza kwa Barcelona kushindwa kufunga katika
hatua ya makundi na jana pia waliambulia sare Turin.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni