Kocha wa Chelsea Antonio Conte
ameviomba vyombo vya habari kumsaidia kuanika ugumu wa ratiba za
mechi zinazomkabili wakati klabu yake ikitinga hatua ya 16 bora baada
ya kuifunga Qarabag kwa magoli 4-0.
Magoli mawili kutoka kwa Wilian,
pamoja na ya mikwaju ya penati ya Eden Hazard na Cesc Fabregas,
yalitosha kuithibitishia Chelsea kuweza kumaliza katika nafasi mbili
za juu za kundi C huku wakiwa na mchezo mmoja.
Kilio hicho cha Conte kinatokana na
kukabiliwa na mchezo dhidi ya Liverpool katika mchezo wa Ligi Kuu ya
Uingereza, Siku ya Jumamosi ikiwa ni siku mbili tu baada ya safari ya
umbali wa mile 5,000 kutokea Azerbaijan.
Mchezaji wa Chelsea raia wa Brazil Willian akifunga goli
Kapteni wa Qarabag akionyeshwa kadi nyekundu na kutolewa nje
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni