.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Desemba 2017

OFISI NZIMA YA MKIKITA WAHAMIA SHAMBANI VIKINDU KUPANDA MCHAICHAI

Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kissui S. Kissui wakibeba miche ya mchaichai wakipeleka kupanda shambani Vikindu. Shmba hilo ni la wanachama wa Mkikita. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange akiwa amebeba mbolea akipeleka shambani.

                                                                               Na Richard Mwaikenda

OFISI nzima ya Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita/Livinggreen), umehamia shamba Vikindu kuanza kampeni ya kupanda mchaichai.

Katika kampeni hiyo ya aina yake iliwashirikisha wakurugenzi, maofisa na wafanyakazi wa mtandao huo ili kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Back to The Land.

Walipofika Block Farming hiyo ya mchaichai, waligawanyika katika makundi mbalimbali ambapo wengine kazi yao ilikuwa kubeba mbegu ya mchaichai, baadhi walisombelea mbolea, kufyeka majani, kuchanganya mbolea kwenye mashimo na wengine kupanda.


Kazi hiyo ilipamba moto hasa baada ya kuhamasishwa na viongozi wakuu ambao pia walishiriki bega kwa bega kubeba mbolea, mbegu na kupanda pia. Hakuna aliyeruhusiwa kukaa bila kazi akiwemo pia mwandishi wa habari hizi, Richard Mwaikenda.

Viongozi walioshiriki kwenye kampeni hiyo ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Dk. Kissui S. Kissui, Mkurugenzi Mtendaji, Adam Ngamange, Mkurugenzi wa Utawala na Mashamba, Catherina, Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth na Mhasibu Mkuu wa mtandao huo, Mshashu na msaidizi wake Samson.

Ofisi kwa siku nzima ilibidi zifungwe kwa siku nzima, ambapo walifanya kazi ya shamba kwa siku nzima ya jana hadi majira ya saa jioni saa 12.
Mkurugenzi wa Fedha wa Mkikita, Elizabeth akipanda mchaichai wakati wa kampeni hiyo
Wafanyakazi wa Mkikita wakiwa wamebeba mbolea ya kupandia mchaichai
Meneja Uhusiano wa Mkikita, Neema (kulia akiwa na Ofisa wa Mradi wa Kuku, Rose wakati wa shughuli ya kupanda mchaichai
                                                      Adam akibeba mbolea kupeleka shambani
                                     Dk. Kissui akiwa amebeba miche akipeleka shambani
                       Eva akifanya usafi kwenye shamba tayari kupanda mchaichai
                                                                     Wakichambua miche ya mchaichai
                                                 Catherina akishiriki vilivyo kwenye shamba hilo
                                                              Adam akichambua miche ya mchaichai
                                               Meneja wa Kijaicos, Mishomari akisafisha shmba
                                                                                                Kazi ikiendelea
Mhasibu Mkuu, Mshahu akishiriki katika kampeni ya upandaji wa mchaichai
                                                                                                            Ni kazi tu
                                      Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth akisaidiana na Matrida
Mhasibu Mkuu msaidizi, Samson akishiriki kusafisha shamba
Hakuna kulala, Mkurugenzi wa mashamba, Catherina akiwa kazini
                                               Sehemu ya shamba lililopandwa mchaichai
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mkikita, Dk Kissui (kulia) akiwapongeza wafanyakazi kwa moyo wao wao wa kujitolea kupanda mchaichai

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni