.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 17 Januari 2018

KELECHI IHEANACHO AWEKA REKODI YA GOLI LA UAMUZI WA TEKNOLOJIA YA VIDEO

Mshambuliaji mwenye asili ya Nigeria Kelechi Iheanacho amekuwa mchezaji wa kwanza katika soka la Uingereza kufunga kwa msaada wa uamuzi wa video wakati Leicester City ikiifunga Fleetwood magoli 2-0 katika mchezo wa raundi ya tatu wa kombe la FA.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City alifunga goli la kwanza baada ya kunasa pande kutoka kwa Islam Slimani, lakini goli lake la pili ndilo lililoivua uamuzi wa kutumika video.

Refa Jonathan Moss alikubaliana na muamuzi aliyetumia video Mike Jones, ambaye alimuambia kuwa guu la Nathan Pond lilimfanya Iheanacho asiwe tena ameotea, na goli hilo kukubaliwa baada ya sekunde 67 kupita tangu kufungwa.
                         Kelechi Iheanacho akifunga goli lililoibua utata na kuamuliwa kwa video
 Refa Jonathan Moss akisikiliza maamuzi kutoka kwa refa msaidizi anayetumia video

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni