.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 23 Februari 2018

ARSENAL YATINGA HATUA YA 16 BORA LICHA YA KUFUNGWA

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema kikosi chake kinaridhika na matokeo ya kunusurika kutolewa na timu ya ndogo ya Ostersunds FK ya Sweden na kutinga hatua ya 16 bora katika Ligi ya Europa.

Arsenal waliokuwa wameshinda magoli 3-0 katika mchezo wa awali ilijikuta ikiduwazwa jana baada ya kutanguliwa kufungwa magoli 2, kabla ya kurejesha goli moja kupitia kwa Sead Kolasinac.

Wageni Ostersunds FK walipata magoli yao kupitia kwa Hosam Aiesh na Ken Sema hata hivyo Aresenal walijikuta wakinufaika na ushindi wa mchezo wa awali na kusonga mbe kwa ushindi wa jumla wa magoli 4-2.
                  Hosam Aiesh akiachia shuti na kufunga mpira uliomshinda kipa David Ospina 
                           Beki  Sead Kolasinac akiachia shuti akifunga goli pekee la Arsenal

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni