.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 23 Februari 2018

POLISI AFARIKI DUNIA AKIDHIBITI FUJO ZA MASHABIKI HISPANIA

Afisa wa polisi mmoja amekufa katika mapigano yaliyoibuka baina ya mashabiki kabla ya mchezo wa Ligi ya Europa baina ya wenyeji Athletic Bilbao na Spartak Moscow katika dimba la San Mames.

Afisa huyo wa polisi kutoka Ertzaintza wa kikosi cha polisi cha kaunti ya Basque ameripotiwa kuwa alikufa kutokana na kupata shambulizi la moyo wakati akidhibiti ghasia hizo za mashabiki.

Fataki na glasi zilirushwa karibu na eneo walilikuwapo mashabiki wa Athletic Bilbao katika tukio hilo la ghasi za mashabiki mitaani lililopelekea pia watu saba kulazwa hospitalini.

Zaidi ya maafisa polisi 500 walipangiwa kusimamia usalama katika mchezo huo na taarifa zinasema kuwa watu watano wamekamatwa kuhuzina na ghasia hizo.
                              Polisi wakimdhibiti mmoja wa mashabiki waliokuwa wakifanya fujo
Fataki zikiwa zinarushwa katika vurugu hizo mitaani zilizoibuka baina ya mashabiki wa timu hizo mbili

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni