.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 27 Februari 2018

AWESO AHAIDI NEEMA KWA WAKANDARASI WA MAJI WAAMINIFU

 Naibu Waziri wa Maji na Umwangiliaji, Mheshimiwa Jumaa Aweso akionja maji yaliyokuwa yakimwagika kutoka kwenye bomba
Naibu Waziri wa Maji na Umwangiliaji, Mheshimiwa Jumaa Aweso akichanganya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kisima
Naibu Waziri wa Maji na Umwangiliaji, Mheshimiwa Jumaa Aweso, akiwa amepanda juu ya kisima cha maji kinachojengwa 

Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Maji na Umwangiliaji, Mheshimiwa Jumaa Aweso ameahidi serikali kupitia wizara ya Maji kulipa kwa wakati wakandarasi waaminifu wanaosimamia miradi ya Maji ili upatikanaji wa Maji uwe endelevu.

Mheshimiwa Aweso ameyasema hayo Jijini Dar kwenye siku yake ya nne ya kikazi alipokuwa akikagua maendeleo ya miradi ya Maji inayotekelezwa na Manispaa pamoja na Miradi ya DAWASCO na DAWASA.

"Wizara ya Maji inajitahidi kutengeneza miradi ya maji itakayomaliza tatizo la Maji kwa wananchi hususani wananchi wenye kipato cha chini hasa vijijini, hivyo mkandarasi atakayefanya kazi yake vizuri na kwa wakati sisi kama serikali hatutasita kumlipa kazi yake kwa wakati"alisema Aweso

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni