Cristiano Ronaldo ametumbukiza
wavuni mpira mara mbili akiisaidia Real Madrid kuichakaza Alaves kwa
magoli 4-0 katika mchezo wa ligi ya La Liga.
Ronaldo alikuwa na nafasi ya kufunga
magoli matatu yaani hat-trick kupitia mkwaju wa penati lakini
alimuachia Karim Benzema ambaye alifunga kwa shuti kali.
Awali Benzema alipika magoli mawili
moja kwa pande la kisigino kwa Ronaldo na lingine akimpatia pasi
Gareth Bale baada ya mapumziko.
Cristiano Ronaldo akimpongeza Gareth Bale baada ya kufunga goli la haraka katika kipindi cha pili
Gareth Bale akianguka baada ya kuchezewa rafu na kusababisha penati iliyozaa goli la nne
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni