.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 24 Februari 2018

LIVERPOOL YAKWEA JUU YA MANCHESTER UNITED

Mohamed Salah amefunga goli katika michezo sita mfululizo wakati Liverpool ikiifunga West Ham magoli 4-1 na kukwea juu ya Manchester United katika msimamo wa ligi.

Emre Can alikuwa wa kwanza kukipatia kikosi hicho cha Jurgen Klopp goli la kwanza kwa mpira wa kona, baada ya mpira uliopigwa na Salah kugonga mwamba.

Salah alifunga goli la pilibaada ya kupatiwa pasi tamu na Alex Oxlade-Chamberlain na kisha baadaye Roberto Firmino akafunga la tatu kwa kosa la kipa Adrian.

Goli zuri la Michail Antonio liliipa West Ham matumaini lakini Sadio Mane ambaye aligonga mwamba mara nyingi akapata nafasi ya kutumbukiza mpira kimiani.
                     Emre Can akiwa amefunga goli la kwanza la Liverpool kwa mpira wa kichwa
   Mohamed Salah akifunga goli la pili la Liverpool kwa shuti la mguu wake hatari wa kushoto

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni