.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 23 Februari 2018

ZABUNI KUBWA YA UJENZI WA HOTELI NA MAENEO YA BIASHARA TBIII YAFUNGULIWA LEO

 Afisa Manunuzi na Ugavi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bi. Margareth Mushi akifungua boksi lililohifadhia zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara katika jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.   
 Nyaraka za tenda za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara kwenye Jengo la tatu la abiria zikiendelea kutolewa ndani ya boksi leo tayari kwa kufunguliwa mbele ya walioomba.
 Boksi lililokuwa limehifadhi nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara kwenye Jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere likiwa tupu baada ya nyaraka hizo kuondolewa tayari kwa ufunguzi leo.
 Nyaraka za zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na kuwekeza katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere zikiwasili jengo ya Jengo la Kwanza la abiria (TB1) ili ziingizwe kwenye ukumbi na kufunguliwa.
 Maboksi ya zabuni mbalimbali za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na uwekezaji katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere yakishushwa kwenye gari kabla ya kuingizwa katika ukumbi wa mikutano wa Transit uliopo jengo la Kwanza la abiria (TB1).

 Wananchi walionunua zabuni za kuwekeza katika ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya biashara kwenye jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere leo wakifuatilia kwa makini wakati wa ufunguaji wa zabuni hizo katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Kwanza la abiria (TB1).
 Afisa kutoka kampuni inayotoa huduma ya mizigo ndani ya viwanja vya ndege ya Nas Airco, Bw. David Ngarapi (anayetazama kamera) akifuatilia zoezi la ufunguaji wa zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na maeneo ya kuwekeza katika maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere zilizofunguliwa leo kwenye ukumbi wa Jengo la Kwanza la abiria (TB1).
Kaimu Mkuu wa Idara ya Manunuzi na Ugavi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Godfrey Kanyama (kushoto) akisikiliza swali kutoka kwa Mama Open Kitchen (Mama Ntilie wa Kishua), wakati wa ufunguzi wa zabuni za ujenzi wa hoteli ya nyota nne na uwekezaji kwenye maeneo ya biashara kwenye Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni