.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 26 Februari 2018

KOCHA PEP GUARDIOLA ATWAA KOMBEA LA KWANZA ARSENAL IKITOTA

Kocha Pep Guardiola ametwaa kombe lake la kwanza akiinoa Manchester City baada ya kuwazidi kila idara Arsenal na kutwaa kombe la Carabao kwa ushindi wa magoli 3-0 katika dimba la Wembley.

City ilizinduka usingizi kutoka kwenye kutolewa kwenye kombe la FA na timu ya ligi daraja la kwanza Wigan Athletic, baada ya kuifundisha soka Arsenal na kuwekeza sasa kwenye ligi kuu ya Uingereza na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika mchezo huo Sergio Aguero alikuwa wa kwanza kufunga goli baada ya beki Shkodran Mustafi kufanya makosa, kisha baadaye Vincent Kompany akaongeza goli la pilia kabla ya David Silva kufunga la tatu.
   Sergio Aguero akifunga goli lake la kwanza kwa mpira wa kumpima urefu kipa wa Arsenal
   Beki wa Manchester City Vincent Kompany akifunga goli la pili katika mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni