Kocha wa Chelsea Antonio Conte
amekiri kuwa haitokuwa kazi rahisi kwa kikosi chake kumaliza katika
nafasi ya nne katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufungwa magoli
2-1 na Manchester United.
Kwa matokeo hayo Chelsea imeporomoka
hadi nafasi ya tato huku Tottenham ikikwea katika nafasi inayoweza
kuipatia nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuifunga
Crystal Palace jumamosi.
Katika mchezo huo Willian alikuwa wa
kwanza kufunga goli, lakini goli hilo lilisawazishwa na Romelu Lukaku na Jesse Lingard
ambaye aliingia akitokea benchi akafunga goli la pili la Manchester
United na kurejea katika nafasi ya pili.
Romelu Lukaku akifunga goli la kwanza la Manchester United dhidi ya timu yake ya zamani Chelsea
Jesse Lingard akifunga kwa kichwa goli la pili la Manchester United kwa mpira wa krosi ya Romelu Lukaku
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni