.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 19 Machi 2018

PEDRO AIPELEKA CHELSEA NUSUFAINALI YA KOMBE LA FA

Goli la dakika za ziada la Pedro limeiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Leicester City na kutinga nusu fainali ya Kombe la FA ambapo watavaana na Southampton katika dimba la Wembley.

Kikosi cha kocha Antonio Conte kiligangamala katika mchezo huo baada ya kutolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelona na kufufua matumaini ya kutwaa kombe hilo katika msimu huu.

Katika mchezo huo Alvaro Morata alifunga goli la kuongoza akinasa pasi ya Willian na kumfunga kipa Kasper Schmeichel kwa utulivu, Leicester ilisawazisha goli hilo kupitia kwa Jamie Vardy katika kipindi cha pili.
                               Mshambuliaji Alvaro Morata akifunga goli la kwanza la Chelsea
                                  Pedro aliyetokea benchi akifunga goli lililoipa ushindi Chelsea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni