.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 19 Machi 2018

RONALDO ACHARUKA LA LIGA APIGA HAT-TRICK YAKE YA 50

Cristiano Ronaldo amefunga hat-trick yake ya 50 katika maisha yake ya soka wakati Real Madrid ikiichakaza Girona kwa magoli 6-3 na kukwea hadi nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ya Hispania La Liga.

Katika mchezo huo Cristiano Ronaldo alifunga goli la kuongoza kutokana na krosi ya Toni Kroos lakini Cristhian Stuani akaisawazishia Girona kwa mpira wa kichwa na kufanya ubao kusomeka 1-1.

Ronaldo akafunga kwa shuti kali na kumtengenezea Lucas Vazquez goli la tatu na kisha kukamilisha hat-trick yake. Staun akaifungi Girona goli la pili naye Gareth Bale akafunga goli la tano, Juanpe akafunga la tatu la Girona kisha Ronaldo akafunga goli la sita.
        Cristiano Ronaldo akiachia shuti na kufunga goli la kwanza katika mchezo huo
              Gareth Bale aliyetokea benchi na kuingia dimbani dakika ya 70 akifunga goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni