.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Aprili 2018

KOCHA JOSE MOURINHO AHITAJI HESHIMA BAADA YA KUIFUNGA MAN CITY

Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amesema kwa kikosi chake kinastahili heshima baada ya kupambana kutoka nyuma kufungwa magoli mawili na kuibuka na ushindi.

Mourinho ametoa kauli hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya wenyeji Manchester City na kuwachelewesha kutangazwa mabigwa wa Ligi Kuu Uingereza.

Kikosi cha United kimekuwa kikikosolewa kwa kutokuwa na kiwango bora chini ya Mourinho, hata hivyo matokeo hayo ya jana katika dimba la Etihad hayatosahaulika.
   Mfaransa Paul Pogba akiwa ameruka juu na kupiga mpira kwa kichwa uliofanya matokeo kuwa 2-2.
   Beki Chris Smalling akiachia shuti lililozaa goli la tatu na kuizamisha Manchester City katika dimba la Etihad.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni