.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 9 Desemba 2013

BALOZI SEIF AWAHIMIZA WANACHAMA, VIKUNDI NA TAASISI ZA CCM KUZIDI KUKITETEA CHAMA CHAO KWA NGUVU ZAO ZOTE


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Uongozi wa Umoja wa Wakerekewa na wana maskani wa CCM wa Umoja wa Askari wastaafu Kijangwani hapo nyumbani kwake katika hafla ya kuwakabidhi msaada kwa ajili yakuimarisha Umoja wao.

                                     Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi Balozi Seif Ali Iddi amewahimiza wanachama  wa Vikundi, Jumuiya na Taasisi za Chama hicho kuendelea kukilinda na kukitetea chama chao muda wote ili kiwe na uhakika wa kuongoza Taifa hili Bara na Zanzibar.


Alisema kazi zinazofanywa na taasisi pamoja na jumuiya hiyo zinaeleweka vyema ndani ya Uongozi wa Chama ngazi zote jambo ambalo viongozi hao wanawajibika kuzisaidia kwa hali yo yote ile.

Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanziubar aliitoa kauli hiyo wakati akikabidhi msaada wa Viti 50, Mabusati 20 na mipira sita kwa Umoja wa wakereketwa na wanamaskani waliochini ya Umoja wa Maaskari wastaafu uliopo Kijangwani Mjini Zanzibar.

Msaada huo ulienda sambamba na Balozi Seif kukabidhi jumla ya shilingi laki tano taslimu kwa Vijana Msimamo Saccos iliyomo ndani ya Umoja huo vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 1,380,000/-.

Aliwapongeza wanachama wa umoja huo kwa uwamuzi wao wa kuazisha taasisi hizo zikiwa na lengo la kuongeza mitaji itakayosaidia wanachama hao kupunguza ukali wa maisha sambamba na kulinda uhai wa Chama chao.

Alieleza kwamba suala la kuanzishwa saccos miongoni mwa wanachama wa vyama vya siasa na hata wananchi katika maeneo mbali mbali nchini limo ndani ya ilani ya CCM na kuendelea kusisitizwa kila mara  na Serikali zote mbili.

“ Kazi mnazozifanya katika jumuia zenu zikiwemo zile za uzalishaji zilizobebwa ndani ya vikundi vya saccos zinaeleweka na kuthaminiwa na Serikali na  ndio maana ukaanzishwa mfuko maalum wa J.K  na A.K “. Alisisitiza Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmshauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif.

Balozi Seif alisisitiza kwamba Serikali wakati wote zinaendelea kuunga mkono juhudi za Wananchi walioamua kuanzisha vikundi vya uzalishaji mali kwa lengo la kujisaidia kimapato.

“ Popote pale mnapooona mnakwama katika kuendeleza shughuli zenu za kila siku tafadhalini msisite kuniona au kuniandikia tutafute namna au mbinu za kuzitatuz changamoto zenu “ Alifafanua Balozi Seif.

Akipokea msaada huo Mjumbe wa Kamati ya Umoja Wakerekewa na wana maskani wa CCM wa Umoja wa Askari wastaafu Ndugu  Ali Ahmada alimshukuru Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif kwa jitihada zake za kusaidia jumuia za Chama hicho.

Nd. Ahmada alisema hatua hiyo ya Balozi Seif mbali ya kuleta faraja kwa wanachama wa jumuiya hizo lakini pia inasaidia kuimarisha nguvu za Chama cha Mapinduzi katika maeneo mbali mbali hapa nchini.

Mapema Mshika fedha wa Vijana Msimamo Saccoc Nd. Ramadhan Saleh Abdulla             { Barongo } alisema saccoc yao imeundwa ili kuwakusanya vijana wapate muda wa kufanya shughuli mbali mbali zitakazosaidia kuwapatia vipato na kuondokana na tabia ya kuzurura mitaani.

Nd. Ramadhan alisema vijana hao wamefikia auamuzi huo baada ya kuelewa kwamba hawatakuwa na uwezo wa kupata ajira kutoka serikalini.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
8/12/2013.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni