.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Desemba 2013

MBIO ZA UHURU MARATHON ZAFANA JIJINI DAR LEO, DKT. BILAL MGENI RASMI


Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 katika Mashindano ya Uhuru Marathon wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi, mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao. Mshindi wa Kwanza ni Jamin Ikai (kutoka Kenya), Steven Selevestor (kutoka Jeshi la Magereza Tanzania) pamoja na Aley Sanka (Tanzania).

Washindi wa Mbio ndefu za KM 42 (wanawake) wakiwa wakiwa wamesimama mbele ya mgeni rasmi, mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao.Mshindi wa  Kwanza ni Thabita Kibet (kutoka Kenya), Naum Jerkosgei (Kenya) pamoja na Banoela Brigton.

Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya Mbio za Uhuru Marathon,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa hotuba yake wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania.


Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara akisoma hotuba yake kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, wakati wa maadhimisho mbio hizo zilizofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru wa Tanzania.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni