.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 9 Desemba 2013

UJENZI WA BANDA KWA AJILI YA SHUGHULI YA MAZISHI YA MANDELA WAANZA

 
Banda kubwa limeanza kujengwa katika eneo la uwanja wa nyumba ya Nelson Mandela litakalotumika kwa ajili ya shughuli ya mazishi yake makubwa kuwahi kufanyika katika historia ya nchi ya Afrika Kusini.

Maandalizi ya mwisho mwisho yanafanyika kabla ya viongozi zaidi ya 70 duniani kuja Afrika Kusini wiki hii kuhudhuria maziko ya mwanasiasa huyo maarufu duniani kwa harakati zake za kudai haki na kupigania amani.

Taarifa zilizotufikia hivi karibuni zinasema Rais Raul Castro wa Cuba na Robert Mugabe wa Zimbabwe nao watakuwemo miongoni mwa wageni kama Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, Prince Charles pamoja na Rais Barack Obama pamoja na wengineo wengi.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni