.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Mei 2014

ANDY MURRAY AGANGAMALA NA KUEPUKA AIBU ILIYOWAKUTA WENYE MAJINA MAKUBWA

Andy Murray ameepuka kutumbukia katika orodha ya majina makubwa yalioanza vibaya baada kuibuka na ushindi wa seti nne dhidi ya Andrey Golubev wa Kazakhstan katika michuano ya Wazi ya Ufaransa.

Muingereza Murray alishinda kwa seti 6-1 6-4 3-6 6-3 dhidi ya Golubev ambaye ni mchezaji namba 53 katika viwango vya dunia katika uwanja Suzanne Lenglen.

Ushindi huo wa Murray ni wa kwanza katika Roland Garros tangu mwaka 2012, baada ya kukosa michuano hiyo kutokana na maumivu ya mgongo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni