.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Mei 2014

WACHEZAJI WAWILI WA TIMU YA TAIFA YA UJERUMANI WANUSURIKA KWENYE AJALI

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Ujerumani itakayo cheza michuano ya kombe la dunia Julian Draxler na Benedikt Howedes, wamepata ajali pamoja na dereva wa mbio za magari za langa langa Nico Rosberg wakati wakipiga picha ya promosheni ya Mercedes.

Rosberg na dereva wa DTM Pascal Wehrlein walikuwa wamewapakia wachezaji hao wa Ujerumani Draxler na Howedes kwenye magari tofauti wakati gari la Wehrlein lilipogonga watu wawili barabarani Kusini mwa Italia, mkoa wa Tyrol.

Rosberg, Wehrlein, Draxler pamoja Howedes hawakujeruhiwa katika ajali hiyo ambayo haikutarajiwa kutokana na barabara hiyo kuwa ilikuwa imefungwa kwa matumizi ili kufanya tangazo hilo la Mercedes.
 















                           Benedikt Howedes                                                             Julian Draxler

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni