.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Mei 2014

LUIS SUAREZ AWATUMIA UJUMBE UINGEREZA NA KUSEMA WATAKUTANA JUNI 19 SAO PAULO

Luis Suarez ametuma ujumbe kwa wachezaji wenzake wa Liverpool walio kwenye kikosi cha Uingereza na kutahadharisha kuwa atakuwa yupo fiti wakati Uingereza itakapochuana na Uruguay katika michuano ya Kombe la Dunia.

Mchezaji huyo bora wa mwaka wa Ligi Kuu ya Uingereza, alifanyiwa upasuaji wa kwenye goti baada ya kuumia katika mazoezi, amewatumia ujumbe mfupi wa maandishi kwa njia ya simu rafiki zake wa Anfield kuwa watakutana Juni 19, huko Sao Paulo.

Daktari wa timu ya Uruguay, Alberto Pan amethibitisha jana kuwa Suarez anaendelea vizuri, baada ya kufanyiwa upasuaji huo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni