.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 18 Mei 2014

KOCHA WA BARCELONA KUACHIA NGAZI, BAADA YA KUFANYA VIBAYA MSIMU HUU

Kocha Barcelona Gerardo Martino ataachia ngazi kuinoa klabu hiyo kwa maridhiano ya pande mbili baada ya kushindwa kuipatia kombe la Ligi ya La Liga.

Barcelona ilikuwa inahitaji ushindi dhidi ya Atletico Madrid ili kutwaa kombe katika mchezo wao wa mwisho hapo jana lakini ikajikuta ikitoka sare ya bao 1-1.

Matokeo hayo yanaifanya Barcelona kumaliza msimu huu bila kutwaa kikombe kikubwa chochote tangu mwaka 2007-2008.

Akiongelea matokeo hayo Kocha Martino, ameomba msamaha kwa kushindwa kufanya vyema, na amewashukuru mashabiki wa klabu hiyo kwa kuwa na imani naye.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni