.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Mei 2014

MWANAMKE MJAMZITO AUWAWA KWA KUPIGWA NA MATOFALI KUTOKANA KUOLEWA NA MWANAUME ASIYEKUBALIKA NA FAMILIA

Mwanamke mwenye ujauzito wa miezi mtatu ameuwawa kwa kupigwa na matofari nchini Pakistan na watu wa familia yake kutokana na kuolewa na mwanaume aliyemchagua mwenyewe.

Mpelelezi Mkuu Rana Akhtar amesema mwanamke huyo Farzana Bibi, alishambuliwa kwa matofali nje ya mahakama kuu huko Lahore High, na watu zaidi ya 12 akiwemo baba yake mzazi na kaka yake.

Farzana alienda mahakamani kumtetea mumewe mpya dhidi ya madai yaliyotolewa na familia yake kuwa alitekwa na mwanaume huyo na kumlazimisha amuoe.

Baada ya tukio hilo baba wa marehemu alijisalimisha, hata hivyo kaka yake na aliyekuwa mchumba wake walikimbia na bado hawajatiwa nguvuni.
                                                                 Mwili wa marehemu Farzana
Mohammad Iqbal akiwa amekaa na mwili wa mkewe Farzana huku akiwa amepigwa na butwaa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni