Kocha wa Manchester United, Louis
van Gaal, amejitetea kwa kutomchezesha mshambuliaji Radamel Falcao
katika kikosi chake kilicholala nyumbani kwa bao 1 dhidi ya
Southampton, kuwa kulitokana na sababu za kiufundi.
Falcao, ambaye alianza kucheza
katika michezo mitano iliyopita jana alikaa benchi na kuishia
kushuhudia Manchester United ikipoteza mechi hiyo ya ligi kuu ya
Uingereza.
Mchezaji huyo wa Colombia anayelipwa
paundi 265,000 kwa wiki, alijiunga na United kwa mkopo akitokea
Monaco, ikiwa ni mwaka mmoja kupita tangu ajiunge na timu hiyo ya
Ufaransa kwa uhamisho wa paundi milioni 50.
Jose Fonte akimdhibiti Robin van Persie asilete madhara langoni



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni