Mgombea urais wa chama cha upinzani
Bi. Kolinda Grabar-Kitarovic amekuwa mwanamke wa kwanza kuwa rais wa
Croatia, kwa kupata ushindi mdogo.
Bi. Kolinda amepata jumla ya
asilimia 50.5 ya asilimia 99 za kura zilizohesabiwa, wakati rais
aliyekuwa madarakani Ivo Josipovic akiwa nyuma kwa kura asilimia
49.5.
Bw. Josipovic amekubali kuwa
ameshindwa katika kinyang'anyiro hicho cha urais na amempongeza
mpinzani wake kwa ushindi aliopata.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni