Rais Francois Hollande anararajia
kuwa mwenyekiti wa mkutano wa mgogoro pamoja na mawaziri wa nchi hiyo
kuhusiana na usalama wa taifa hilo baada ya kutokea mashambulizi ya
kigaidi wiki iliyopita Jijini Paris.
Mkutano huo umeitishwa huku kikiwa
na maswali juu ya ni vipi wapiganaji hao wanaharakati wa Kiislam
waliofahamika na mamlaka za nchi hiyo waliweza kutekeleza uvamizi na
mauaji hayo Jijini Paris.
Mashambulio hayo ya kigaidi katika
jarida la vibonzo la Charlie Hebdo, shambulio lingine la polisi
katika tukio tofauti pamoja na katika duka kubwa la bidhaa la kosher
yalisababisha vifo vya watu 17. Zaidi ya watu milioni 1.5
waliandamana Jijini Paris jana kuonyesha mshikamano.
Umati wa watu Jijini Paris katika maandamano ya kuonyesha mshikamano
Rais Hollande akimkumbatia mwandishi
wa jarida la Charlie Hebdo, Patrick Pelloux



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni