Baraza la Mawaziri la nchini Jamaica
limeidhinisha muswada utakaohalalisha matumizi kidogo ya bangi.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa
taifa hilo la marastafarian, ambalo linatumia mmea huo kama sehemu ya
imani yao, sasa kuweza kuvuta bangi bila kuvunja sheria za nchi.
Muswada huo pia unatoa fursa ya
kutolewa leseni za kulima bangi, mauzo na usambazaji kwa ajili ya
kutumika kama dawa na tiba mbalimbali.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni