Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa
Mtaifa ametoa wito kwa Myanmar kushutumu kitendo cha Kiongozi wa
Kitaifa wa dhehebu la Buddha wa taifa hilo kumuita mjumbe Maalum wa
UN kuwa ni kahaba.
Mkuu huyo wa Haki za Binadamu, Zeid
Ra'ad Al Hussein amesema kauli iliyotolewa na kiongozi wa Buddha,
Ashin Wirathu inachochea chuki.
Kauli hiyo Wiradhu ilikuwa inamlenga
Mjumbe huyo wa Korea Kusini, Bi. Yanghee Lee, ambaye alikuwa ziarani
Myanmar wiki iliyopita akijaribu kushughulikia tatizo la kundi dogo
la jamii ya Kiislam.
Wirathu aliwahikufungwa jela karibu
muongo mmoja kwa kuchochea vurugu za kupinga Uislam.
Mjumbe UN Bi. Yanghee Lee


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni