Mtu anayejiita kiongozi wa Boko
Haram, amesema katika video kuwa wapiganaji wake ndio walioendesha
shambulio mbaya la mauaji ya watu katika mji wa Baga nchini Nigeria
mapema mwezi huu.
Mtu huyo ambaye amesema kuwa yeye ni
Abubakar Shekau amesema watu hao wameuwawa kama walivyoagizwa na
mungu wao, na kutishia kufanya mashambulio zaidi.
Baadhi ya taarifa zinasema watu
wapatao 2,000 wameuwawa katika mashambulizi yaliyofanyika Baga, hata
hivyo serikali ya Nigeria inapinga na kusema waliokufa ni watu 150.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni