Raia wa Mali muislam ambaye
aliwanusuru wateja kushambuliwa na mtu mwenye silaha mwenye kufuata
itikadi kali za kiislam katika duka la bidhaa la Paris Kosher mwezi
huu amepatiwa uraia wa Ufaransa.
Lassana Bathily, 24, ambaye ni
mfanyakazi wa duka hilo kubwa la bidhaa alikuwa kwenye chumba cha
kuhifadhia bidhaa wakati mtu mwenye silaha Amedy Coulibaly alipovamia
duka hilo na kuua watu wanne.
Bathily ambaye alifikiri haraka na
kuzima vyumba vya friji katika duka hilo na kisha kuwaficha wateja,
amekabidhiwa paspoti na medali ya ushuja na Waziri Mwandamizi wa
Ufaransa.
Shambulio hilo la Jijini Paris
limeuwa watu 17, huku idadi kubwa walikuwa katika ofisi ya jarida la
vibozo la Charlie Hebdo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni