Kamanda Mwandamizi wa waasi wa
Uganda, Dominic Ongwen amewasili Jijini The Hague kukabiliana na
makosa ya uhalifu wa kivita.
Ongwen, ambaye ni kamanda
anayeogopwa wa waasi hao wa Lord's Resistance Army (LRA), alikuwa
akishikiliwa na Marekani katika nchi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati
mapema mwezi huu.
Nchi ya Uganda imekubali kuwa Ongwen
ashtakiwe katika mahakama ya Kimataifa ya uhalifu (ICC), licha ya
kuwa imekuwa mstari wa mbele wa kuikosoa mahakama hiyo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni