Wapiganaji wanaohisiwa ni wafuasi wa
kundi la Boko Haram nchini Nigeria, wameteka makumi ya watu baada ya
kufanya uvamizi katika nchi jirani ya Cameroon.
Mamlaka zimesema wengi wa waliotekwa
katika uvamizi huo uliofanyika katika kijiji kimoja mpakani, ni
watoto.
Vyanzo vya usalama vimesema
wanakijiji wanne waliojaribu kujitetea kukabiliana na washambuliaji
waliuwawa.
Boko Haram wanamiliki miji na vijiji
kaskazini-mashariki mwa Nigeria, na wameanza kuwa tishio kwa nchi
jirani.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni