Waziri wa Afya wa Mali amesema nchi
hiyo sasa haina tena virusi vya Ebola, baada ya kupita siku 42 bila
ya kuwa na tukio jipya la mgonjwa wa ugonjwa huo.
Waziri huyo Ousmane Kone amenukuliwa
akisema kuwa anaitangaza siku ya jana kuwa ndio mwisho wa mlipuko wa
Ebola nchini Mali.
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha
nchi tatu za Afrika ya Magharibi zilizoathiriwa mno na Ebola matukio
ya kesi mpya za wagonjwa yamepungua.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni