Mawaziri wa Umoja wa Ulaya
watakutana hii leo kujadili tishio la ugaidi barani Ulaya, kufuatia
mashambulio ya kigaidi.
Ulaya ipo katika tahadhari ya juu,
baada ya jaribio la ugaidi lililoshindwa nchini Ubelgiji, na
shambulio hatari Jijini Paris lililouwa watu 17.
Pia mawaziri hao watajikita katika
kujadili uhusiano wa Ulaya na Urusi katika kujaribu kutafuta ufumbuzi
wa mgawanyiko mkubwa wa serikali Ulaya kuhusina na namna ya
kuichukulia nchi hiyo baada ya vitendo vyake dhidi ya Ukraine.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni