Brazili na Uholanzi zimewaita
mabalozi wao waliopo nchini Indonesia, baada ya kuchukizwa na
serikali ya nchi hiyo kupuuzia maombi ya nchi hizo na kutekeleza
adhabu ya kifo kwa kupigwa risasi watu sita waliotiwa hatiani kwa
dawa za kulevya wakiwemo raia wawili wa nchi hizo.
Waliotiwa hatiani na kuuwa mbali na
raia wa Brazili na Uholanzi, pia yupo raia wa Vietnam, Malawi,
Nigeria, pamoja na raia mmoja wa Indonesian, ikiwa ni hukumu za
kwanza za kifo kutekelezwa chini ya rais mpya Joko Widodo.
Nchi ya Indonesia inasheria kali
dhidi ya dawa za kulevya na rais Widodo, aliyeingia madarakani Oktoba
mwaka jana amewakera wanaharakati kwa kuonyesha kuunga mkono adhabu
ya kifo licha ya kuonekana ni mwanamageuzi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni