.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 18 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA AFRIKA, WENYEJI EQUATORIAL GUINEA WABANWA NA CONGO, GABON YAICHAKAZA BURKINA FASO

Fainali za michuano ya kuwania kombe la Mataifa ya Afrika zimeanza jana nchini Equatorial Guinea kwa kuwashuhudia wenyeji wa michuano hiyo wakilazimishwa kwenda sare ya kufungana bao 1-1 na Congo. 

Katika mchezo huo wa ufunguzi, wenyeji Equatorial Guinea ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 16 likifungwa na Nsue Lopez. Bao hilo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. 

Hata hivyo kipindi cha pili Congo walijibu mapigo na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha katika dakika ya 87 mfungaji akiwa ni Bifouma Koulossa.
 Katika mchezo mwingine wa michauano hiyo ya Mataifa ya Afrika, Burkina Faso  walikiona cha moto baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Gabon. 

Katika mchezo huo, Gabon walijipatia mabo yao kupitia kwa Pierre-Emerick Aubameyang katika dakika ya 19. 

Bao la pili la Gabon lilipatikana katika kipindi cha pili mfungaji akiwa ni Malick Evouna aliyefunga bao dakika ya 72. 

Kwa matokeo hayo, Gabon ndiyo inayoongoza kundi A kwa kupata pointi 3 baada ya wenyeji Equatoria Guinea na Congo kutoka sare ya kufungana bao 1-1

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni