Kocha wa Congo Claude LeRoy amekasirishwa na kitendo cha timu yake kukaa barabarani kwa muda mrefu katika basi lenye joto wakati wakielekea katika mchezo wao wa ufunguzi wa Kombe la Mataifa ya Afrika.
Katika mchezo huo Congo ilitoka sare
ya bao 1-1 na wenyeji Equitorial Guinea, baada ya kufanikiwa
kusawazisha katika dakika za mwisho.
LeRoy amesema kwa kawaida safari ya
kwenda uwanjani ilikuwa ikiwachukua dakika 12, lakini jana
iliwachukua dakika 65 wakiwa kwenye foleni katika basi ambalo halina
viyoyozi wakati joto likiwa nyuzi joto 40.
Kocha huyo wa Congo amesema kulipaswa
kuwepo kwa jitihada za kuondoa msongamano wa magari ili timu ziweze
kufika mapema uwanjani na kutoa wito kwa CAF kuchukua hatua kuhusiana
na suala hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni