Papa Francis atasherehekea misa ya
wazi na mamilioni ya watu nchini Ufilipino katika Jiji la Manila.
Inakadiriwa watu milioni tatu,
wameshakusanyika katika eneo la Rizal Park ikiwa ni saa mbili kabla
ya misa hiyo kuanza.
Miaka 20 iliyopita zaidi ya watu
milioni 5 walihudhuria misa iliyoongozwa na Papa John Paul II nchini
humo.
Vatican imesema Papa Francis
atatumia misa hiyo kuwaombea wahanga wa kimbunga Haiyan, ambacho
kiliiathiri nchi hiyo mnamo mwaka 2013.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni