.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 18 Januari 2015

NDUGU WAWILI CHERIF KOUACHI NA SAID KOUACHI WAZIKWA KWA SIRI NCHINI UFARANSA

Cherif Kouachi, mmoja wa waliohusika katika kundesha mashambulizi ya kigaidi katika jarida la vibonzo vya dhiahaka la Charlie Hebdo, amezikwa katika kaburi lisilo na alama chini ya ulinzi mkali.

Maafisa wa nchi hiyo wamesema Kouachi amezikwa usiku katika mji wa nyumbani kwao wa kitongoji cha Gennevilliers, Jijini Paris.

Kaka yake ambaye alishirikiana naye katika mashambulizi hayo yaliyouwa watu 12, Said Kouachi naye alizikwa usiku Ijumaa katika eneo la siri mashariki mwa mji wa Reims.

Awali meya wa Reims alikataa kutoa eneo la kuzikia lakini alilazimwishwa kufanya hivyo kisheria.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni