Wabunge wawili wa Kiambu wamemsihi
rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto to kupuuzia wito wa
kufanya mazungumzo na muungano wa CORD, kwa madai kuwa hawana hoja
za msingi.
Mwakilishi wa Wanawake wa Kiambu,
Annah Nyokabi na Mbunge wa jimbo la Lari, Mburu Kahangara wamesema
kitendo cha CORD kusisitiza mazungumzo ni mbinu za kuionyesha dunia
uongozi wa serikali ya Jubilee umeshindwa.
Kahangara amesema kuwa iwapo Uhuru
atakubaliana na matakwa ya kambi ya upinzani, kutapelekea uwezo wake
wa kufanya maamuzi sahihi kuhojiwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni