.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 23 Januari 2015

POLISI KENYA WAUWA MAJAMBAZI SITA KWA KUWAPIGA RISASI JIJINI NAIROBI

Majambazi sita wamepigwa risasi na kufa jana usiku baada ya polisi kuzima mipango yao ya wizi katika eneo Membley, barabara ya Ruiru-Kahawa Jijini Nairobi.

Majambazi hao wote wanaume walikuwa kwenye gari aina ya saloon, iliyokuwa ikifuatiliwa na polisi ambapo mmoja wao aliyekuwa na silaha aina ya AK-47 alitoroka baada ya kulifyatulia risasi gari la polisi.

Afisa wa kitengo cha uhalifu amesema walipata taarifa kuwa majambazi hao walikuwa wanapanga kuweka kizuizi barabarani na kuwaibia wenye magari watakaopita barabara hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni