Watu 56 akiwemo mtoto mdogo wamekufa
kaskazini magharibi mwa Msumbiji kutokana na sumu iliyowekwa kwenye
pombe ya kienyeji ijulikanayo kama 'phombe'.
Mkurugenzi wa Afya katika Mkoa wa
tete Carla Mosse, ameiambia redio Mocambique watu 39 bado wamelazwa
hospitali hii leo, baada ya kupata madhara ya pombe hiyo iliyokuwa na
sumu.
Wahanga wote wa tukio hilo akiwemo
mtoto wa miaka miwili, walishiriki maziko siku ya Ijumaa asubuhi, na
kisha kunywa pombe ya kienyeji inayotengenezwa kwa kutumia mbegu za
mtama.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni