Mamlaka nchini Nigeria zimesema
idadi ya watu waliopoteza maisha yao katika shambulio lililofanywa na
wapiganaji wa kundi la Boko Haram, wiki iliyopita ni zaidi ya watu
150.
Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo
amesema idadi hiyo inahusishapia magaidi wengi, ambao waliushambulia
mji Baga katika jimbo la Borno na kukabiliana na upinzani kutoka kwa
jeshi.
Maafisa wa eneo hilo walikadiri kuwa
shambulio hilo limesababisha vifo vya watu 2,000.
Serikali ya Nigeria imekuwa
ikilaumiwa kwa kushusha idadi ya vifo katika kuonyesha tatizo la Boko
Haram kuwa sikubwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni