Video imetolewa ikionyesha mwanaume
mweusi akipigwa risasi na afisa wa polisi Marekani, wakati akitoka
nje ya gari huku mikono yake akiwa amenyoosha juu.
Mwanaume huyo Jerame Reid alikuwa ni
abiria katika gari lililoamriwa kusimama na polisi wa Bridgeton, New
Jersey, kwa kosa la kukatiza wakati alama ya kusimama ikionyesha.
Kabla ya polisi kumfyatulia risasi
mtu huyo afisa mwingine alimtahadharisha mwenzake kuwa ameona silaha
kwenye gari hilo.
Tukio hilo linafuatia maandamano ya
miezi kadhaa kuhusiana na mauaji wa Marekani weusi wasio na silaha
yaliyofanywa na polisi weupe Jijini New York na Ferguson, Missouri.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni