Watu wapatao 18, wamekufa katika
mapigano baini ya polisi na waandamanaji katika maeneo tofauti ya
Misri.
Maafisa wa nchi hiyo wamesema
miongoni mwa waliokufa ni maafisa polisi watatu, ambapo pia makumi ya
waandamanaji pia wamejeruhuiwa.
Mapigano hayo yamefuatia kifo cha
mwanaharakati katika maandamano katika Jiji la Cairo siku ya
jumamosi.
Maandamano hayo yaliitishwa
kuadhimisha miaka minne ya vuguvugu la nguvu ya umma iliyomuondoa
madarakani rais Hosni Mubarak mwaka 2011.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni