.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 24 Machi 2015

MAHAKAMA YA SENEGAL YAMUHUKUMU KIFUNGO MTOTO WA RAIS WA ZAMANI

Mahakama nchini Senegal imemuhukumu mtoto wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Abdoulaye Wade kifungo cha miaka sita jela baada ya kupatikana na hatia ya kujihusisha na rushwa.

Mtoto huyo Karim Wade pia amepigwa faini ya dola milioni 230, kwa kujitajirisha visivyo halali wakati wa utawala wa miaka 12 wa baba yake.

Karim Wade mwishoni mwa wiki alichaguliwa kuwa mgombea wa urais kwa chama cha upinzani cha PDS.

Rais wa Senegal Macky Sall wiki iliyopita alionya kuwa serikali yake haitovumilia jaribio lolote la kuhatarisha usalama wa nchi, baada ya mahakam kutoa hukumu yake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni