.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 6 Mei 2015

MAREKANI YAANZA KURUHUSU HUDUMA YA FERI KATI YAKE NA CUBA BAADA YA MIAKA 50

Kivuko kinatarajiwa kuanza kufanya shughuli ya kuvusha watu kutoka Florida kwenda Cuba, kwa mara ya kwanza tangu miaka 50 kupita baada ya serikali ya Marekani kuridhia huduma hiyo mpya ya usafiri.

Huduma za kivuko hicho zilisitishwa baini ya mataifa hayo majirani, baada ya Marekani kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Cuba mnamo mwaka 1960.

Hata hivyo Marekani ilitangaza kurejesha mahusiano ya kidiplomasia mwezi Desemba mwaka jana, kwa kuondoa vikwazo na idadi kadhaa za vivuko zimepewa leseni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni